Ezra 5:3-6
3 aWakati ule Tatenai mtawala wa ng’ambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao waliwaendea, wakawauliza, “Ni nani aliyewapa ruhusa ya kujenga tena Hekalu hili na kurudishia upya kama lilivyokuwa?” 4Pia waliwauliza, “Je, majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani?” 5 bLakini jicho la Mungu wao lilikuwa likiwaangalia wazee wa Wayahudi, nao hawakuzuiliwa kujenga mpaka taarifa ikaandikwa kwa Dario na majibu yake kupokelewa. 6 cHii ni nakala ya barua ile Tatenai, mtawala wa ng’ambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao maafisa wa ng’ambo ya mto Frati waliyompelekea Mfalme Dario.
Copyright information for
SwhKC